Watu sita waaga dunia katika ajali Kendu Bay

Na, Carren Omae

Watu sita wamefariki dunia na wengine kumi kujeruhiwa kwenye ajali iliyotokea jioni hii kwenye barabara ya Kendu Bay-Katito, Kaunti ya Homabay. Ajali hiyo iliyohusisha gari la abiria na jingine dogo imetokea kilomita moja kutoka mjini, Kendu Bay.
Mkuu wa Polisi Kaunti ya Homa Bay, John Omusanga amesema waliojeruhiwa wanatibiwa katika hospitali iliyo karibu.
Kulingana na walioshuhudia ajali hiyo, walioaga dunia walikuwa abiria.